Naanza yangu nudhuma
Kwa adabu na heshima
Kumueleza yatima
Hana wa kumtizama
Sio kosa la yatima
Majanga kumuandama
Ni mipango ya karima
Waja wake kutupima
Hufurahika yatima
Akionewa huruma
Hupata kutabasama
Kupendwa na wote umma
Tumpendeni yatima
Kwa kumtendea wema
Ili kwenye pepo njema
Tuweni naye hashima
Unapompa furaha
Wamfariji jeraha
Kwani hilo si mzaha
Ni msiba wa daima
Kuna wengi mayatima
Wanaotamani kusoma
Ila shida darahima
Na pia pa kuegema
Kunao wengine watu
Wasiokuwa na utu
Kuwatesa wasubutu
Bila ya hata huruma
Yatima tusimtese
Wala tusimnyanyase
Kichwani tumpapase
Ndivyo asema hashima
Tusiwaone ni nuksi
Wao ni kama sisi
Tusiweni wabinafsi
Tuishi nao kwa wema
Wengine kwenye jalala
Mahali wanapolala
Na pia chao chakula
Nashindwa hata kusema
Wanakosa matibabu
Maradhi yawaadhibu
Kwa kweli wapata tabu
Hawana wao salama
Wengine wanauawa
Mabinti kunajisiwa
Vile vile wanauzwa
Jamani huu ni unyama
Nauliza langu swali
Kula ya yatima mali
Jamani ni haki kweli?
Tumuogope karima
Malipo ni duniani
Hilo tia maanani
Sijitie matesoni
Kwa kudhulumu yatima
Kesho siku ya hesabu
Pia kunao adhabu
Kwa wanaowapa tabu
Watoto walo yatima
Na hayo yote ni tisa
Kumi ninasisitiza
Yatima kutomliza
Ili tupate salama
Siendelei zaidi
Kukoma inanibidi
Na japo kwenye fuadi
Nina mengi ya kusema
Kikomoni nimefika
Kalamu chini naweka
Jina langu kwa hakika
Farwa shariff mi nasema
Good job
LikeLike
Thanks dear 😘
LikeLike
a commanding voice.edge of the seat reading…excellent
LikeLiked by 1 person
Thanks so much
LikeLike
Mashallah it’s nice and a moving one. Thanks for sharing
LikeLike
Shukran ukhty
LikeLike
Nice one mashaAllah
LikeLike
Shukran
LikeLike
Let those with ears take heed, well said ms.
LikeLiked by 1 person
Shukran jazila 😃
LikeLike